Taarifa kutoka Bodi ya Ligi Kuu inaeleza kuwa
"Mchezaji Clatous Chama wa klabu ya Simba amefungiwa michezo mitatu (3) na kutozwa faini
ya Sh. 1,000,000 kwa kosa la kumkanyaga kwa makusudi mchezaji Nickson Kibabage wa klabu ya Yanga
mchezo wa Derby Aprili 20, 2024.
Adhabu hii ni kwa kuzingatia Kanuni ya 41:5(5.2) ya Ligi Kuu kuhusu Udhibiti kwa Wachezaji."
Chama atakosa mchezo wa Simba dhidi ya Mtibwa Sugar, Tabora United na Azam FC.