top of page

KATIBU MKUU WA UMOJA WA MATAIFA ANTONIO GUTERRES APIGWA MARUFUKU KUINGIA ISRAEL, YASEMA HAKULAANI SHAMBULIO LA IRAN.

Na VENANCE JOHN


Israeli imetangaza kuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres kuwa mtu asiyetakiwa nchini Israel.


Nchi hiyo imempiga marufuku kuingia katika ardhi ya Israeli kwa kile ilichokieleza kuwa ni Katibu mkuu huyo kutokosoa na kulaani shambulio la Iran dhidi ya Israel. Waziri wa mambo ya kigeni wa Israeli, Israel Katz amemtaja Guterres kama mtu anayetoa msaada kwa magaidi, wabakaji na wauaji.


Hatua hiyo inakuja baada ya mataifa ya magharibi ikiwamo Marekani, Ujerumani, Uingereza na Ufaransa miongoni mwa nyinginezo kulaani shambulizi la Iran kuishambulia Israel kwa kile kilichoelezwa ni kulipiza kisasi dhidi ya Israel kwani imewauwa viongozi wa makundi ya kipiganaji inayoyaunga mkono.


Opmerkingen


Msasa Media
  • Instagram
  • Facebook
  • X
  • Youtube
  • TikTok

Follow, like, comment, and share

Tel. +255758379300
Mbezi Dar es saalam

bottom of page