top of page

ALIYEKUWA MKUU WA MKOA SIMIYU AKITUHUMIWA KUMLAWITI MWANAFUNZI WA CHUO KIKUU AACHIWA HURU NA MAHAKAMA

Na VENANCE JOHN


Mahakama ya Hakimu Mkazi jijini Mwanza imemuachia huru aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Dkt. Yahya Nawanda katika kesi ya kulawiti iliyokuwa ikimkabili. Uamuzi huo ulikuwa wa kesi ya jinai namba 1883/2024, yenye kosa la kulawiti, na uliosomwa na hakimu, mkazi mfawidhi wa mahakama hiyo Erick Marley.


Katika uamuzi huo, hakimu Marley amesema mahakama hiyo baada ya kupitia maelezo ya ushahidi na vielelezo imejiridhisha kuwa hakukuwa na muunganiko wa ushahidi unaoweza kumtia mshtakiwa Dk. Nawanda hatiani na hivyo kumwachia huru.

Comments


Msasa Media
  • Instagram
  • Facebook
  • X
  • Youtube
  • TikTok

Follow, like, comment, and share

Tel. +255758379300
Mbezi Dar es saalam

bottom of page